WCB Watoa Tamko La Rich Mavoko Kwenda Kujisajili BASATA Kwa Mara Ya Pili

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Rich Mavoko ameamua kujitoa rasmi katika Label yake iliyokuwa ikimsimamia ya WCB kwa ajili ya mgogoro wa mkataba aliopewa.

Baada ya kutoka WCB, Mavoko alionekana akienda kushtaki katika Baraza la Sanaa Tanzania ambapo pia alidaiwa kwenda BASATA kwa ajili ya kujisajili upya pamoja na kwamba alishasajiliwa chini ya WCB.

download latest music    

WCB wameibuka na kudai taarifa za Msanii huyo kwenda kujisajili BASATA sio sawa kwani tayari ameshasajiliwa chini ya Label hiyo mapema mwaka huu.

Kwenye mahojiano na GPL, Meneja kutokea WCB, Sallam SK amesema hayo alipokuwa akieleza ushirikiano uliyipo kati ya WCB na Baraza hilo kwa sasa.

Suala la kusema hatushirikiani na BASATA hilo litakuwa si la kweli na sisi tunashirikiana nao sana kuna vitu vinatokea bahati mbaya. Lakini ukiangalia wasanii wetu wote wamesajiliwa BASATA na hamna yeyote ambaye hajawahi kujisajili. Hata juzi kati hapa ilisemekana kuwa Rich Mavoko ndio alienda BASATA akajisajili, hapana!, kashasajili kupitia WCB, actually mwezi wa saba mwaka huu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.