Wema Afika Mahakamani Baada Ya Kufanyiwa Upasuaji Nchini India

Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu alifika mahakama ya Kisutu siku ya jana baada ya kutoka nchini India Kwenye matibabu na kufanyiwa upasuaji.

Wema anakabiliwa na kesi ya kutumia madawa ya kulevya na kesi yake imekuwa ikiendelea kusikilizwa tangu mwaka jana.

download latest music    

Wema alifika na wafanyakazi wake wawili wanaokabiliwa na kesi ya kutumia dawa ya kulevya katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,  wataanza kujitetea Juni 19, mwaka huu.

Wema na wenzake walipaswa kuanza kujitetea leo Juni 13 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba,  na kwa upande wa mawakili ni Cosstantine Kakula wa Serikali na Wakili wa Utetezi, Albert Msando.

Lakini hata hivyo watuhumiwa hao walishindwa kujitetea siku ya jana kutokana na kwamba Hakimu Simba alikuwa na kazi nyingine na kesi imeahirishwa hadi Juni 19, mwaka huu ambapo washtakiwa wataanza kujitetea.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.