Wema Angeshindwa Kulipa Faini Ya Milioni 2 Ningemlipia Mimi- Kajala

Muigizaji wa Bongo movie Kajala Masanja amefunguka na kuweka wazi kuwa endapo msanii mwenzake Wema Sepetu angeshindwa kulipa faini ya milioni 2 basi angamlipia yeye.

Miaka ya nyuma Wema alishawahi kumtupia Kajala faini ya shilingi milioni 13 ambayo iliweza kumsaidia kutokwenda jela kwa miaka saba kutokana na kesi yake ya utapeli.

download latest music    

Lakini tangu miaka hiyo Wema na Kajala walikuja kugombana na kuwa maadui wakubwa na juzi ilikuwa zamu ya Wema ambaye alihukumiwa kwenda jela kwa mwaka mmoja au kulipa faini ya shilingi milioni 2.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Kajala ambaye kwa sasa yupo nchini Dubai, alisema kuwa kama angetakiwa kusaidia kumlipia Wema faini hiyo asingekuwa na tatizo, angemlipia.

Ningejua na kuwa na hakika Wema hawezi kulipa hiyo faini, ningemlipia hata kama ni kwa kukopa hizo pesa, lakini mimi sikuwepo nchini wakati Wema anahukumiwa.

Lakini pia Kajala ameeleza kusikitishwa kwake na taarifa zinazosambaa kuwa amemtelekeza rafiki yake Wema:

Jamani mimi naona watu wanasema sikuonekana mahakamani, lakini hawajui kama nipo au sipo, hata hivyo kama ingehitaji faini ambayo kubwa kwa kweli mimi nisingeshindwa hata ya kukopa ningemlipia.

Sio kwamba sikuwa napenda kwenda mahakamani kuungana naye, kulikuwa na vitu vinaendelea kwa upande wangu hivyo ikaniwia vigumu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.