Wema: Hamisa ni Mdogo Wangu Lakini Mazoea Yamezidi

Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu amefunguka na kuongelea uhusiano wake na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto huku akidai kuwa ni mdogo wake ila mazoea yalizidi hivyo aliamua kumuweka kando.

Siku za nyuma Wema na Hamisa walikuwa marafiki sana kwa miaka mingi na hata ni mara nyingi Hamisa amekuwa akisikika akimuita Wema dada yake.

download latest music    

Lakini urafiki huo uliingia shubiti siku za nyuma baada ya Wema kutaka kumtumia watu wampe kichambo Hamisa na hata kudai sababu ya wawili hao kutofautiana ni baada ya kumsikia Hamisa akimsema maneno mabaya.

Kwenye Interview yake na Global Tv, Wema amefunguka kuwa Hamisa ni mdogo wake lakini alizidisha sana mazoea hivyo ilibidi amuweke kando ili heshima iwepo:

Mimi hamisa ni kama mdogo wangu, hivyo yaani waga nasema kila siku Lakini sometimes mazoea yakizidi sana sijui huwa inaleta mushkeri kwaiyo inabidi kila mtu abaki kwenye mipaka yake ili ajue hapa natakiwa nipitilize au hapa nisipitilize”.

Watu wengi walihusisha Wema kugombana na Hamisa na Diamond lakini Wema aliweka wazi kuwa aligombana na Hamisa kwa sababu alimsikia anamsema vibaya kwa watu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.