Wema: Zari Alimuacha Diamond Kwa Mambo Aliyomfanyia Huko Nyuma Sio Kisa Mimi

Muigizaji wa Bongo movie mwanadada Wema Sepetu amefunguka na kusema anaamini Zari alimuacha Diamond kwa mambo yao waliyotofautiana kipindi cha nyuma lakini sio kisa yeye alimkumbatia.

Baada ya Zari kutangaza kumuacha Diamond alifanya Interview na BBC Swahili na aliweka wazi kuwa amemuacha aliyekuwa mpenzi wake supastaa wa Bongo fleva Diamond kwa sababu ya yeye kukumbatiana na Wema kwenye party.

download latest music    

Wema na Diamond walikuwa pamoja kwa miaka kadhaa huko nyuma na wamekuwa na tabia ya kuachana na kurudiana hata Diamond amedaiwa kuchepuka kwa wapenzi wake wapya na Wema hivyo alivyoonekana tu Wema wanakumbatiana ikaonekana tayari.

Lakini Wema amekataa tuhuma za Zari kuwa amemuacha kisa yeye Kwenye Interview aliyofanya wikiendi iliyopita na Bongo 5 Wema Alitalia maneno haya juu ya suala hilo:

Zari alikuwa ana sababu nyingi sana za kupanick za nyuma za Diamond za mambo yao wenyewe lakini sio hiyo ya juzi ya mimi kumkumbatia Diamond kama rafiki atakuwa ana jingine”.

Lakini pia Wema aliweka wazi kuwa pamoja na yeye na Diamond wameachana kipindi kirefu kilichopita lakini bado wana chemistry ambayo haiwezi kuisha.

Wema alipotakiwa kumshauri kitu chochote Zari alifunguka na kusema kuwa hawezi kuwa mshauri wa Zari kuhusu Mahusiano yake na Diamond.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.