Wolper Akana Kutambulisha Mwanaume Nyumbani

Mwanadada mkongwe kabisa katika tasnia ya filamu nchini ambae pia ni  mjasiriamali Jackline Wolper , amefunguka na kusema kuwa hajawahi kumtambulisha mwanaume yoyote nyumbani kwao kwa sababu alishaona kuwa hakuna ambae anasifa za kutambulishwa kwao au kumuoa yeye.

Mwanadada huyo ansema kuwa wanaume wengi aliokuwa nao ilikuwa ni kwa ajili ya kupeana starehe na kula raha lakini hakuwa na umakini wa kumpekleka nyumbani kwa sababu hawakuwa na sifa za kuwa wakwe.

download latest music    

Akionge na Global Online Tv, Jackline Wolper ambae alikuwa na usiku mzuri wa Stylish Night kwa ajili ya kuji-brand yeye na biashara yake alisema kuwa  pamoja na kwamba ameshapiata kiampenzi na wanaume wengi sana wa nje na ndani ya tasnia ya sanaa lakini hakuwahi kumpeleka mwanaume hata mmoja kwao kwa sababu walikuwa na lengo la kufanya starehe tu.

Sijaolewa na siajwahi kutolewa mahali wala kumtambulisha mtu, kwanini nimtambulishe mwanaume?

Akiendelea kuongea Wolper alisema kuwa anayoyafanya katika mitandao ni kwa sababu mama yake hayupo huko ila angekuwepo wala asingethubut.u

kwa kuwa nafanya vitu vya kijamii , najaribu kuepukana na baadhi yta mambo, mahusiano yangu mnayoyaona katika mitandao huwa ni ya kujifurahishga tu kwakweli na ndo maana mnaona nachiachia sana lakini endapo mama yangu angekuwa katika mitandao ya kijamii wala  nisingejaribu kufanya hivyo, lazima niwaheshimu wazazi wangu.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.