Wolper Amsifia Faiza Kwa Picha Yake Ya Uchi Adai Asijali Maana Wabongo Washamba

Muigizaji wa Bongo movie na mwanamitindo Jacqueline Wolper ameibuka na kumpa tano rafiki take Faiza Ally kwa picha ile ya uchi na kudai asijali maana wabongo ni washamba tu kwa kutoelewa maana ya picha ile.

Mwishoni mwa wiki iliyopita Faiza aliwashangaza watu wengi baada ya kuamua kurusha picha iliyomuonyesha akiwa uchi kabisa huku sehemu zake za siri zikiwa wazi wakati akizaa leba mtoto wake wa kiume. Baada ya pica hiyo kusambaa ilizua gumzo sana na kusababisha picha hiyo kuenea mtandaoni kama moto wa kifuu.

download latest music    

Baada ya picha hiyo watu wengi walimjia juu Faiza huku mastaa wa mziki kama Snura akimuomba Faiza aitoe picha ile kwa kuwa ilikuwa haimdhalilishi tu yeye kama mwanamke bali wanawake wote maana mambo yanayotokea leba yanapaswa kuwa ya siri kabisa.

Wolper alipohojiwa na kituo kimoja cha habari ili aweze kupima uzito kwenye suala linalo-trend hivi sasa ambalo ni picha ya uchi ya Faiza, Wolper alidai anawashangaa wait wanaomponda Faiza aliyeposti picha hiyo hivi karibuni kwenye ukurasa wake wa Instagram wakati yeye amevutiwa sana na kitendo hiko na iko siku atamuiga.

Wabongo ni washamba sana ushamba ndio unawasumbua sio kitu kingine kabisa, sioni ubaya wa ile picha hata kidogo eti katudhalilisha sasa pale kamdhalilisha nani? Mimi nimefurahi mno na binafsi ipo siku nitamuiga endapo nitajaaliwa kupata mtoto wangu mwenyewe”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.