Wolper Atabiri Kifo Cha Bongo na Kuwataka Wasanii Waache Unafki

Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Masawe maarufu kama Jacqueline Wolper ameibuka na kuweka wazi kuwa Bongo movie imekufa na kuwataka wasanii waache unafiki.

Wolper alijizolea umaarufu miaka ya nyuma kutokana na uhodari wake katika sekta ya kuigiza lakini siku za hivi karibuni amegeukia ujasiriamali na kujiingiza Kwenye ufundi cherehani.

download latest music    

Wolper ametoa povu zito kwa wasanii wenzake kupitia ukurasa wake wa Instagram huku akiwaasa waache unafki ili sanaa isonge mbele Lakini pia ametabiri kifo cha tasnia hiyo:

Natamani Bongo movie Tupendane saana yani saaaaana, kiukweli na syo kinafk kiasi kwamba ata mtu akitokea akamuongelea bongo movie vibaya basi wote tusimame nae paka ajute kwanini kafanya hlo tukio, lakini maskin ya Mungu mchawi wetu kafa atujui kaburi lake tukamuombe Radhi atusamehe tuwe huru..yani Mtu akikosea ndio kwanza Tunakandamiza nakuonyesha wasioliona lile kosa ichi ni kilio nanimsiba mkubwa R.i.p Bongo movie.
Acha nipambane na cherehani zangu niangalie nijinsi gani nakomboa mafundi chereani na Tuheshimike Tanzania hope Mafundi chereani amtoniangusha na amtokua wanafki”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.