Wolper Awatolea Mate Cardi B na Rihanna

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Jacqueline Wolper ameibuka na kuweka wazi kuwa anawakubali sana wasanii wawili wakubwa ambao ni Cardi B na Rihanna angependa siku moja awavalishe.

Wolper anamiliki duka lake la mavazi ama boutique inayojulikana kama House Of stylish na amewavalisha wasanii kadhaa na nguo zake anazovaa anahusika mwenyewe kuzishona.

download latest music    

Wolper amefunguka na kuweka wazi ndoto zake kubwa katika sekta ya fashion ni kufika mbali kimataifa zaidi mpaka kuwavalisha wasanii wakubwa duniani.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo5 Wolper amesema moja ya ndoto zake ni kuja kuwavisha wasanii wakubwa Marekani kama Rihanna na Cardi B.

Rihanna na Cardi B ndio wana swagger zangu kwa hiyo ni watu ambao ninatamani kuwavalisha, na ninajua one day yes..

Mitandao inaonyesha na inathibitisha kwamba nimebuni kitu one week akaja akavaa Rihanna, nimebuni kitu one day, kesho yake anakuja anavaa Cardi B”.

Kibongo Bongo Wolper ameshawavalisha mastaa kama msanii wa Bongo movie Aunty Ezekiel na wasanii wengine kama Gigy Money na wengineo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.