Wolper: Sarah wa Harmonize Ana Matatizo Ya Kisaikolojia, Anahitaji Msaada

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu, Jacqueline Wolper amemtolea povu zito hasimu wake namba moja Sarah mzungu ambaye ni mpenzi wa Ex boifrendi Harmonize.

Siku ya jana Wolper na Sarah waliongia kwenye vita ya maneno kwenye mitandao ya kijamii baada ya Sarah kwa mara nyingine kumtuhumu Wolper kwa kumtaka Harmonize.

download latest music    

Sarah alimpa onyo Wolper na kumtaka aache kuongea na Harmonize ambapo alitupia screenshots za meseji ambazo amekuwa akimtumia Harmonize huku imeonekana wazi kuwa hamjibu.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Wolper amemjia juu Sarah huku akidai lazima atakuwa na ugonjwa wa kisaikolojia na kutaka watu wampe msaada:

Hivi ni vitu vya kuona huruma na kusamehe kwa sababu yule dada ana wasi wasi maskini anaamini kwamba nitachukua chombo chake wakati mimi muda huo sina lakini anajua mimi ni kiboko yake kwaiyo anaamini kuwa nitamchukua kitu ambacho siwezi mimi nikipita nimepita siwezi kumchukua tena na cha muhimu yule dada anahitaji mtu wa kumpima akili yule dada sio mzima ana matatizo ya kisaikolojia haiwezekaani kitu kidogo analipuka vile”.

Wolper amefunguka kuwa akaunti yake ilikuwa hacked na mtu ambaye ali hack alikuwa anatuma meseji kwa watu mbali mbali dm ikiwemo kwa Harmonize.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.