Yasemekana Lulu Michael Aachiwa Huru
Habari zilizosambaa sana kwa siku ya tarehe 13 May zinasema kuwa mwanadada Elizabeth Lulu Michael ameachiwa huru na kwamba inasemekana kifungo chake kimepatiwa msamaha wa raisi hivyo mwanadada huyo yuko huru.
Ingawa habari hizi hazinathibitika bado , lakini chanz cha habari zinasema kuwa siku ya jana Lulu Michael alitolewa gerezani na kusemakana kuwa kwa sasa yuko huru.
Bado kumekuwa na mkanganyiko wa maneno kuhusu kuac hiwa kwake ingawa hakuna picha ya karibuni iliyomuonyesha msanii huyo akiwa huru lakini sababu za kutoka kwake gerezani zimekuwa nyingi huku wengine wakisema kuwa ni msamaha wa raisi, wengine wakisema kuwa rufaa yake imefanikiwa huku wengine wakisema kuwa ameatiwa kifungo cha nje.