Young Dee Aukacha na Uongozi Wake.
msanii wa muziki wa rap nchini young dee amefunguka na kusema kwa sasa amecahana na ule uongozi wake alikuwa chini yake hapo awali ana anategemea kuanza kufanya kazi pekee yake.Young dee anasema kuwa kwa sasa amefungua kampuni yake mwenyewe ambayo itakuwa ikisimamamia kazi zake za sanaa na kampuni hiyo itakuwa chini ya uongozi wake yeye mwenyewe.
Young dee anasema kuwa wiki ijayo atatoa wimbo wake mwenyewe , wimbo ambao ndip utakuwa wimbo wake wa kwanza kutoka katika kampuni yake ambayo ataanza kufanya nayo kazi kupitia wimbo huo unaokuja.
Wikiendi hii pia kumekuwa na picha zilizosambaa katika mitandao ya kijamii zikimuonyesha msanii huyo akiwa na mwanamke pembeni yake huku wakiwa katika mazingira ya kufunga ndoa.