Young Lunyo Afungukia Tetesi za Kulimendea Penzi la Wolper

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayechipukia kwa kasi ya ajabu Young Lunyo anayeunda kundi la OMG amefunguka na kumuongelea msanii wa Bongo movie Jacqueline Wolper na uwepo taarifa za mahusiano kati yao.

Wolper ni moja kati ya mastaa wa Bongo movie ambaye mara kwa mara amekuwa akihusishwa na wanaume wadogo kiumri maarufu kama viben-10 au serengeti boys kwaiyo watu walivyoona wana mazoea sana hasa kwenye Instagram utaona Young Lunyo anamposti sana Wolper.

download latest music    

Bongo 5 wanaripoti kuwa Young Lunyo amekana tetesi hizo na kudai hazina ukweli wowote ila zimesababishwa na ukaribu ambao walionao wawili hao kwa ajili ya mazoea waliyojijengea:

Wolper ni dada yangu ambaye ananipa sapoti katika muziki wangu na nilivyopata hizo taarifa sikujisikia vizuri kwa kweli, nilijisikia vibaya kwa kuwa tunaheshimiana sana, sijashangaa sana kwa maana ni msanii kwaiyo lazima ingekuwa Ivyo”.

Lakini Young Lunyo amedai kwa upande wake tayari ana mpenzi wake lakini pia Wolper amedai ana mpenzi lakini asingependa kumuweka wazi kwa sasa mpaka muafaka utakapowadia.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.