Z Anto Kuja na “Mpaka Naogopa” Baada Ya Kimya Kirefu

Msanii mkongwe wa Muziki wa Bongo fleva aliyewahi kutamba na vibao vyake kama vile ‘Binti kiziwi’ na ‘Mpenzi jini’ Z Anto ametangaza kurudi kwenye  gemu baada ya kimya kirefu.

Baada ya kufanya vizuri sana miaka ya nyuma Z Anto alikaa kimya kwa muda mrefu mpaka mwaka jana alipoachia Wimbo Mpya ‘Cheza unapochezaga’ ambao haukuweza kumrudisha vizuri Kwenye chati.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Z Anto amesema kwamba wimbo wa kwanza ‘Kacheze Unakochezaga’ ulikuwa wakuombea msamaha kwa watanzania kutokana na ukimya wake na baada ya kuona amekubaliwa anajipanga kuachia wimbo wake mpya alioupachika jina ‘Mpaka Naogopa’.

Ni project mpya inakuja soon, wimbo nimefanya kwa Mazuu ni ngoma kali sana ambayo itakuja kuwaonyesha mashabiki kwamba mimi ni nani katika muziki wa BongoFleva, nimefanya vingi lakini pia naweza kubadilika.

Kacheze Unakochezaga ni wimbo ambao niliuachia kuwaomba mashabiki msamaha baada ya kukaa muda mrefu bila kuachia wimbo. Na wimbo wangu mpya ‘Mpaka Naogopa’ ni wimbo ambao utawafanya mashabiki wangu waamini kwamba Z Anto ni mtu au msanii tofauti sana katika tasnia ya muziki na ni tofauti na hao wengine ndio maana nikasema mimi siji kushindana kwa sababu nina kitu tofauti“.

Z Anto amewataka mashabiki zake wanaenda mkao wa kupata burudani kwani ana akiba zaidi ya nyimbo ya 20.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.