Zamaradi Adai Uvumilivu Ulimshinda Akaamua Kumwaga Povu Mtandaoni

Mtangazaji wa Wasafi Tv Zamaradi Mketema amefunguka baada ya bifu lake na mrembo Hamisa Mobetto na kudai uvumilivu ulimshinda ndio maana akamwaga povu lile Instagram.

Siku chache zilizopita Zamaradi na Mobetto waliingia kwenye vita kali ya maneno baada ya kugombana kisa nguo ambayo Zamaradi alivaa kwenye 40 ya mtoto wake.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Zamaradi amefunguka na kudai kuwa alifunguka na kuongea mambo Yale kwa sababu alishindwa kuvumilia kusemwa vitu vya uongo ili hali ukweli upo.

NI kweli nimeongea na kuweka vitu wazi lakini yule sio mimi ila kuna muda  tu vitu vinakufika kooni na kushindwa kuvivumilia kwa sababu hata uongo unapozungumzwa sana hugeuka na kuonekana kama ndio ukweli na Watanzania ni watu wa kuchukua kitu kama kilivyo na kila mtu hongea lake na sikuongea kama ni povu bali nilitaka kuweka wazi ili watu waelewe nini kinaendelea”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.