Zamaradi Afunguka Kuhusu Mapenzi na Mume wake, ni Kila Kitu Kwake.

Ikiwa jana ni siku muhimu kwa familia ya zamaradi mketema kutokana na sherehe kubwwa iliyokuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu  ya 40 ya mtoto wake aliyejifungua siku kadhaa zilizopita, mwanadada Zamaradi alipata fursa ya kumtambulisha mumu wake katika sherehe hiyo na kujikuita akifunguka mengi kuhusu baba huyo.

Akiongea mbele ya umma Zamaradi anasema kuwa mume wake ni kama baba kwake kutokana na ukweli kuwa amekuwa  mtu muhimu , anaemuelewa na kumjali kwa kila kitu tangu amekuwa nae  katika maisha yake.

download latest music    

Zamaradi pia amesema kuwa siri kubwa ambayo wengi inawezekana walikuwa hawaijui ni kwamba , mume wake ndie alikuwa akimkanda na maji ya moto kwa kipindi chote alichojifungua mtoto wake huyo wa kiume.

Zamaradi pia amesema kuwa kwake sio shida kuzaa na kuendelea kuongeza familia na mwanaume huyo hata kama anawatoto watatu tayari.

Amenikubali kama nilivyo na kunipenda na mimi nimemkubali kama alivyo na kumpenda pia,mpaka hapa tulipo tuna familia pamoja na tunategemea kuongeza familia pamoja ,nataka tu kumwambia kuwa nina kupenda sana na asante kwa kila kitu.

kitu ambacho wengi hamjui ni kwamba kipindi chote cha kujifungua nimekuwa nikikandwa na yeye na hii kutokana na kwamba hakukuwa na mzazi wa kunikanda mimi, wazazi wangu wote walishatangulia mbele ya haki.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.