Zamaradi Mketema Kuoneka Mubashara Ndani ya Wasafi Tv

Muigizaji mkongwe Zamaradi Mketema amethibitishwa kuanza kuonekana live kama mtangazaji katika redio station na televisheni station mpya ya Wasafi Tv and Radio inayomilikiwa na msanii Diamond Platnumz.

Suala hili Limekuja baada ya ukimya mrefu aliokuwa nao Zamaradi Kwenye anga ya utangazaji. Mara baada ya Zamaradi kumuacha aliyekuwa mpenzi wake na Baba watoto wake mkurugenzi wa Clouds Fm Ruge Mutahaba na kuolewa na mwanaume mwingine mwaka jana Zamaradi aliacha kazi Clouds Fm pia.

download latest music    

Mapema mwaka huu kuna tetesi zilisambaa kuwa Zamaradi atajiunga kwenye redio mpya ya Diamond lakini zilikuwa ni tetesi tu lakini mpaka jana usiku tunaweza kuthibitisha kuwa ni taarifa za kweli kabisa na mpaka hivi sasa Zamaradi yupo na timu nzima ya WCB.

Hamornize alithibitisha taarifa hizi kwa kuweka picha kwenye mtandao wake wa Instagram na kusindikizwa na ujumbe wa kumkaribisha Zamaradi ndani ya Wasafi Tv:

Let’s go Mama Juju welcome to th Family Wasafi Tv”.

Zamaradi na Diamond Pamoja na timu nzima ya WCB wapo visiwani Zanzibar kwa ajili kufanya zoezi la kusaka vipaji vipya vya watangazaji ambao watafanya kazi katika kituo hicho kipya cha Wasafi tv.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.