Zari Amchana Diamond Baada Ya Kugoma Kuwaona Watoto Wao

Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz ameingia vitani na mzazi mwenzake mfanyabiashara Zarinah Hassan baada ya kumtuhumu kwa kutokwenda kuwaona watoto wao na kutojua wanaishije mpaka hivi sasa.

Diamond na Zari walikuwa Kwenye Mahusiano kwa miaka minne na zaidi lakini mwaka huu mwezi wa Pili Zari alivunja Mahusiano yao baada ya kuchoshwa na michepuko ya Diamond lakini alisisitiza kuwa watabaki marafiki kwa ajili ya watoto wao.

download latest music    

Lakini sasa urafiki huo umeelekea ukingoni kwani Zari amempa makavu Diamond na kumtaka aende akawaone watoto wao kwani watoto hawajamuona Baba yao kwa miezi kadhaa sasa.

Zari amemtolea povu hilo Diamond Kupitia ukurasa wake wa Snapchat ambapo amewatolea maneno pia mameneja wake na kuwataka wamshauri msanii wao akawaone watoto wao kwani watakuwa wameshaanza hata kumsahau Baba yao:

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.