Zari Amtolea Nje Msanii Kutoka Kenya Aliyejitolea Kumuoa

Mfanyabiashara maarufu kutoka Uganda aliyeweka makazi yake nchini South Africa Zarinah Hassan ‘Zari the Bosslady’ ambaye pia ni baby mama wa msanii Diamond Platnumz ameweka wazi kuwa hana mpango wowote wa kuanzisha mahusiano ya kimapenzi na mwanaume wowote kwa hivi sasa.

Zari amefunguka hayo alipokuwa anafanya mahojiano na BBC Swahili London, Uingereza ambapo alifunguka mengi kuhusiana na mahusiano yake na Diamond lakini pia aliongelea mipango yake ya mbeleni kimapenzi hasa.

download latest music    

Wiki iliyopita msanii wa nyimbo za Injili kutoka Kenya anayejulikana kama Ringtone alifunguka na kuweka hisia zake hadharani juu ya Zari baada ya kusema anataka kumuoa na hata kuongeza kuwa yupo tayari kupeleka ng’ombe 42 nchini Uganda kama mahari baada ya Diamond kumzalisha watoto na kushindwa kumuoa.

Tangu Zari aachane na Diamond kumekuwa na tetesi nyingi kuwa anatoka na wanaume kadhaa hasa kumekuwa na mwaname anayeitwa Mr. X ambaye ilisemekana kuwa alichukua nafasi ya Diamond lakini Zari amezima tetesi hizo zote baada ya kusema hana mpenzi na hahitaji kuwa na mtu yoyote kwa sasa:

Hapana sitafuti huwa na mahusiano, mapenzi yakitokea yanatokea kwa hivyo siwezi kusema sitakuwepo kwenye mahusiano tena ila kwa sasa najiangalia mwenyewe na maisha yangu na watoto wangu kwaiyo ntapumzika kwa sasa”.

Lakini Zari alifunguka na kusema kuwa ni ngumu kwake kuwa na mahusiano kwa sasa kwani hataki kuwachanganya watoto wake kwa kumuona na mwanaume tofauti kila siku. Hivyo wale wote waliokuwa wanategemea kupata nafasi ikiwemo Ringtone wakajaribu kwingine kwani Zari kasema hataki mahusiano kwa sasa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.