Zari Anunua Ndinga Lenye Thamani Ya shilingi Milioni 172

Mfanyabiashara maarufu na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan amethibitisha kuwa yeye ni Bosslady kweli baada ya kuweka wazi kuwa amenunua gari aina ya Range Rover lenye thamani ya shilingi milioni 171,337,500.

Zari alitangaza mpango wake wa kununua gari hilo wiki chache zilizopita na hatimaye wikiendi hii alilianika gari hilo jipya na kuliweka Kwenye mitandao ya kijamii.

download latest music    

Mara baada ya kuweka gari hilo kuna habari zilizuka kuwa amenunuliwa gari hilo na mpenzi wake taarifa alizozikana na kuweka wazi kuwa amenunua gari lile kwa hela zake mwenyewe.

Lakini pia Zari ameweka wazi mipango yake ya kuanzisha Food franchise kama vile KFC au McDonalds.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.