Zari Asitisha Mahojiano na Vyombo Vya Habari Baada Ya Maswali Ya Diamond na Hamisa Kutawala

Mfanyabiashara maarufu na mzazi mwenza wa msanii Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari The Bosslady’ amesitisha mahojiano yake na kituo cha redio cha Capital FM na stesheni zote baada ya kuchoshwa na maswali ya maisha yake binafsi.

Zari amekuwa kwa wiki moja sasa nchini Uganda na amefanya media tour katika vituo mbali mbali kwa ajili ya kutangaza party yake ya Zari All White Party, lakini Jana kabla ya shoo yake alisitisha mahojiano na kituo cha Capital FM kwa like alichodai anaulizwa maswali ambayo yapo kibinafsi Sana na hapendelei kuyajibu bali yuko interested na kuongelea kazi zake zaidi kuliko maisha yake binafsi.

download latest music    

Kutokana na drama zinazoendelea mtandaoni kati ya Diamond, Zari na Hamisa kila radio station aliyoenda Zari amefunguka mengi sana juu ya kinachoendelea kati yake na Diamond na usaliti aliofanyiwa na mzazi mwenzake huyo baada ya kuzaa na Hamisa miezi michache iliyopita.

Kupitia page yake ya snapchat Zari aliujulisha umma wa Uganda kuwa hataweza kuendelea na mahojiano na vituo mbali mbali vya redio kutokana na kukwepa drama zinazokuja na maswali yanayoulizwa na waandishi wa habari kuhusu maisha yake binafsi kwani anachotaka kuzzungumzia ni Zari, watoto wake na biashara zake tu.

Nimeamua kuhairisha kufanya interview na vituo vyote vya habari kutokana na kuulizwa maswali ambayo mengi ni binafsi sana na sipo tayari kwa drama zinazofanyika na ninaamini kuwa drama ni kwa ajili ya watu wenye drama ila mimi naangalia maisha yangu watoto wangu na  biashara zangu, lakini natarajia kumuona kila mtu usiku wa lao kwa ajili ya Zari All White Party”.

Kwenye interview zote alizofanya Zari nchini Uganda amekuwa muwazi sana kwa kile kilichotokea kati yake na Diamond na Hamisa jambo lililozua maneno maneno mengi kwenye mitandao ya kijamii.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.