Zari: Diamond Ameniomba Sana Msamaha Baada Ya Kuchepuka

Zarinah Hassan maarufu kama Zari The Bosslady amefunguka na kuweka wazi kuwa mzazi mwenzake staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz alimuomba sana msamaha baada ya kuchepuka.

Katika Interview yake na Global Publishers, Zari amekiri kuwa tangu Diamond amsaliti na kuzaa na Hamisa Mobetto mwaka jana amemuomba sana msamaha na hata Babu Tale kuenda South Africa juzi juzi ilikuwa ni kuomba radhi.

download latest music    

Babu Tale alikuja Pretoria, alitaka turudiane na Diamond kwa ajili ya watoto, sikuona ubaya katika hilo, lakini mambo ya mapenzi hapana tena, watu haohao wa karibu walipaswa kumuonya Diamond wakati anafanya mambo yake kwa sababu anaamini walifahamu kila kitu.

Wangemwambia Diamond aache mambo aliyokuwa anayafanya. Kufufua penzi kwa sasa ni vigumu sana, wameshachelewa. Mimi nawaheshimu sana, na ndiyo maana hata Babu Tale alipokuja nilimkaribisha vizuri. Sina ubaya na mtu yeyote, hata ndugu zake Diamond“.

Lakini Zari amesisitiza kuwa taarifa zilizoenea kuwa wawili hao walirudiana Diamond alipoenda Sauzi sio za kweli kwani hawakulala hata chumba kimoja:

Diamond alikuja kuwaona wanawe. Alilala chumba kingine na mimi nikalala chumbani kwangu. Tuliongea kuhusu kuwa karibu lakini ni kwa ajili ya watoto tu. Kwa sasa sina uhusiano wowote.  Nimeyaweka kando mambo hayo, nachoangalia ni kulea watoto wangu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.