Zari Kwa Mama Diamond ” Fanya Tuhame Madale Guest House Tumwachie Mwanao”.

Mzazi mwenza na mpenzi wa Msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari the Bosslady’ ameendelea kukaa kwenye vichwa vya habari baada ya kuachia bomu jingine.

Tangu Hamisa aachie picha zilizomuonyesha alikuwa anajiachia Nyumbani kwa Diamond Madale na hata ofisini kwa Diamond sasa imekuwa fasheni kwa wasichana kujipiga picha wakiwa Madame na kisha kuzisambaza mtandaoni.

download latest music    

Wiki iliyopita kuna msichana anayetambulika kwa jina la Mila ambaye video yake akiwa Nyumbani kwa Diamond, Madale kusambaa mtandaoni na kusababisha tafrani hadi kupelekea Zari kupaita Madame Guest house yaani nyumba ya kulala wageni.

Zari ameonyeshwa kuwa bado ana kinyongo na Diamond kwa tuhuma za wanawake kwenda kujiachia Nyumbani kwao Madale wakati yeye akiwa nchini South Africa.

Lakini pia inaonekana mpaka sasa ishu hiyo ya Diamond kupeleka wasichana kulala Madale bado inamkera Zari kwani ameendekea kuiongelea baada ya kumwandiki mama mzazi wa Diamond kuwa wahame Madale guest house na wamuache mwanaye ambaye ni Diamond peke yake, Zari alimwandiki Mama Diamond ujumbe huu:

Fanya tuhame guest house tumwachie mwanao”.

 

 

Kabla ya sakataa hili la wiki iliyopita halijaishaa vizuri Zari kamuongeza Zari na skendo jingine la kukumbatiana na Wema na mpaka sasa haijajulikana vipi uhusiano wa Diamond na Zari upoje ingawa Diamond ameshasema hawezi kuiacha familia yake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.