Zari na Hamisa Wajibu Tuhuma za Kupata Umaarufu Kupitia Kuzaa na Diamond

Wazazi wenza wa Mwanamuziki Diamond Platnumz, Mfanyabiashara Zarinah Hassan ‘Zari The Bosslady’ na muigizaji Hamisa Mobetto wameongelea tuhuma walizorushiwa kuwa wanapata umaarufu zaidi kupitia kuzaa na Diamond.

Hamisa na Zari wana ufanano wa kitu kimoja tu nacho ni kuwa wote wamezaa na Diamond lakini zaidi ya hapo ni maadui wakubwa kupita kiasi hilo lilidhihirika mwezi uliopita pale wote walipokuwa na shoo nchini Uganda ambapo waliishia kurushiana maneno ya kashfa mtandaoni hadi kufikia hatua ya kutukanana.

download latest music    

Diamond ni msanii mkubwa sana sio tu Tanzania bali hata nje ya Tanzania kwenye nchi nyingi za Africa hata nje ya bara la Africa kumekuwa na maneno mengi yanayosemwa huku watu wakidai kuwa warembo hawa wanafurahia hizi kiki za kuwa na Diamond kwani na wao wanapata umaarufu wakujulikana.

Kuna maneno yamekuwa yanasemwa kuwa Zari yupo na Diamond sio kwa ajili ya pesa bali ya umaarufu kwani inasemekana kuwa anapenda sana fame na kiki.

Zari ali[ohojiwa na Millard Ayo Tv alifunguka kuhusu tuhuma hizo kama ifuatavyo;

Naweza kusem ndiyo na hapana, ndiyo kwa sababu sahivi tumekuwa couple yenye nguvu (power couple) watu wanapenda kutuongelea sana na vitu kama hivyo hata hivyo kabla kulikuwa kuna watu walikuwa wanamjua Diamond mimi hawanijua na kuna watu walikuwa wananijua mimi na Diamond hawamjui kwaiyo nahisi tumesaidiana kujulikana”.

Hamisa naye alifunguka tuhuma hizo kwani tangu amezaa na Diamond amekuwa akisafiri nchi kama Kenya, Uganda, na Nigeria, Dubai kwenda kufanya shughuli mbali mbali:

Habari hiyo ni ya kweli kwani Diamond ni mwanamuziki mkubwa lakini mwanzo nilivyokuwa na mimba nilikuwa sijui nini kitatokea lakini tangia hapo sijapata jina kubwa tu au umaarufu lakini pia changamoto ambazo zinanilazimisha nipambane maana maisha nayo magumu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.