Zari na Hamisa Wameingia Tena Kwenye Bifu Kali Baada Ya Kurushiana Maneno Mazito Mtandaoni

Wazazi wenza wa Msanii Diamond Platnumz na Hamisa Mobetto wameingia tena kwenye bifu zito baada ya kila mmoja kumrushia maneno mwenzake mtandaoni.

Kisa cha ugomvi huo kilianza siku chache zilizopita baada ya Zari na Hamisa kujikuta wana sherehe siku moja nchini Uganda Jana hapo ndipo mashindano yalipoanza huku kila mmoja akijinadi atakuwa juu zaidi huku wakisaidiwa na timu.

download latest music    

Party hizo mbili zilifanyika Jana usiku kwenye kumbi mbili tofauti lakini kwa wakati mmoja. Baada ya party hizo picha zilianza kusambaa mtandaoni huku kila mmoja akijitahidi kuonyesha kuwa alikuwa na nyomi kubwa kuliko mwenzie.

Baada ya muda warembo hao wawili walianza kurushiana maneno katika mtandao wa Snapchat na Instagram huku kila mmoja  akimtambishia mwenzie kuwa amepata mafanikio zaidi ya mwenzake lakini pua walifikia hadi hatua ya kurushiana maneno ya kashfa.

Zari ameibuka akumrushia maneno haya Hamisa kupitia kurasa yake ya Snapchat:

Kuna tofauti kubwa Kati ya tembo na mbu, baraka juu ya  baraka Asante Mungu, Watu wenyewe ni maslay cartoons, wezi wa wanaume za watu wanataka waishi kwa kutegemea child support lakini wapi hawawezi kushindana na mimi, wameenda mpaka kisutu lakini wameambulia patupu”.

Baada ya kurushiwa maneno hayo Hamisa alishindwa kuvumilia kwani na yeye amefunguka ya kwake na kumrushia Zari madongo:

Siwezi kubishana na bibi yangu, Mimi nina umri wa binti yako wa kwanza unemzidi mama yangu miaka 3…Mama yangu amenifundisha kuheshimu wakubwa walionizidi alafu ungejiamini wako angetulia…alaku wewe endelea kulilia kuvalishwa pete wakati mwenzako mume wa mtu tayari”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.