“Sitaki Kusikia Kuhusu Diamond Wala Mama Yake”. Amesisitiza Zari Kuwa Amemuacha Diamond Kweli Sio Kiki

Zari amerudi tena Kwenye headlines za mitandao ya kijamii baada ya kutoa povu zito baada kuulizwa kuhusu uhusiano wake na Baba watoto wake Diamond Platnumz.

Uhusiano wa Zari na Diamond umekuwa gumzo kila kona tangu wiki iliyopita siku ya Valentine’s ambapo Zari alitangaza kuwa amemuacha Diamond kwa sababu ya kuendekeza michepuko.

download latest music    

Siku ya jana kupitia Instalive ya Instagram Zari alitoa povu kali pale alipoulizwa swali kuhusu Diamond na shabiki wake.

Zari alizungumza haya kuhusu Diamond na familia yake:

Kuna mtu kaniuliza kuwa kosa gani la mwisho ambalo Diamond alikufanyia mpaka ukaamua kumuacha? Naomba niseme mara ya mwisho kuanzia sahivi huu ukurasa ni wangu na nitaongelea kuhusu mambo yangu binafsi yaani mambo ya Zari haihusiani na Diamond wala Mama yake wala sitaongelea alichokifanya au wanawake wake malaya wake waliochoka hapana kwaiyo hapa mnaniongelea mimi na watoto wangu”.

Lakini pia Zari amefunguka na kusisitiza ni kweli amemuacha Diamond na taarifa zote kuwa ni Kiki zinazoendelea kusambaa mtandaoni sio za kweli.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.