Akaunti ya Zari Yadukuliwa Mapema Leo.
Akunti ya instagram ya mwanamama Zari the Bossy leo mapema baada tu ya kuweka birthday wishes za mtoto wake wa kike imedukuliwa na kufutwa kila kitu katika akaunti hiyo.
Mwanadada huyo ambae hivi karibuni tu aliweza kufikisha followers zaidi ya 1milion anaripotiwa kutoonekana wala kupatikana kwa sasa katika mtandao huo kutokana na wajanja hao kumfanyia mchezo huo mchafu.
Hata hivyo watu wake wa karibu wamethibitisha hilo huku wakisema kuwa wanafanya kila liwezekanalo hili kutatua tatizo hilo.