Alichosema TID kuhusu Chid Benz

Msanii khalid mohamed maarufu kama ‘Top In Dar’ (T.I.D )   ambae ni mmoja kati ya wasani wakongwe katika muziki wa Tanzania na kila unapoongelea wasanii wa zamani basi uwezi kuacha kumuongelea msanii huyu wa kiume.Msanii huyo ambae  hivi karibuni pia alikumbwa na kashfa ya matumizi ya dawa za kulevya akikuwa muwazi na  alikubali kusaidiwa ili kuacha matumizi ya dawa hizo amefunguka na kuongea kuhusu msanii mwenzie mkongwe Chid Benz.

Akiwa mmoja wa wasanii wakongwe ambao kwa kipindi kile walishuka kwenye muziki Chid Benz bado anaonekana kusuasua kuimarika katika kazi hiyo kutokana na kukumbwa na kashfa za kutumia na kuuza madawa ya kulevya richa ya kupelekwa rehab kwa matibabu.Msanii huyo hivi karibuni ametoa wimbo unaojulikana kwa jina la ‘Muda’ akimshirikisha Q-Chillah na umekuwa ukifanya vizuri  katika vituo mbalimbali vya radio na televisheni.

download latest music    

T.I.D alipoulizwa kuhusu msanii mwenzie alionyeshwa kukerwa na tabia ya Chid ya kukataa kusaidika na kusema kuwa anapoteza muda wa watu wanaotaka kumsaidia , ‘unampeleka dentention ,unamfunga pingu,akitulia unamuachia unamwambia nenda kafanye muziki wako” alisema T.I.D.

Hata hivyo akiongea na Clouds E  kuhusu kazi zake za kisanii msanii T.I.D  mweney  lebel   inayojulikana kama Radar Entertainment , anasema kuwa wapo vizuri  pamoja na kwamba waliondokewa na msanii wao mmoja mkubwa, Ngweah ambae alifariki miaka michache iliyopiya lakini  wapo imara pia uongozi ni mzuri na wameshasajili wasanii wengine kutoka nje na ndani ya nchi akiwepo Babu wa Kitaa pamoja na Kr Mullah ambao pia wote wanafanya vizuri chini ya menejiment hiyo na wanategemea mambo mazuri. Pamoja na kutetereka na kushuka kimziki kwa mudamfupi  wa nyuma uliopita kwa sasa T.I.D amekuwa akifanya vizuri katika nyimba zake mpya huku zin gine akiwashirikisha na kushirikishwa pia na  wasanii wenzie kama Dudubaya, Tofy na wengine wengi.

Pia ni chini ya menejiment hiyo ya Radar Entertainment ndipo alipotokea msanii chipukizi  Billnas ambae anafanya vizuri  sana katika muziki wa  bongo.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.