Alikiba aeleza kwanini Barakah The Prince alitemwa na lebo ya Rockstar4000

Barakah The Prince alikua amesainiwa Lebo ya kimataifa la Rockstar4000 kabla ya kuihama lebo hio. Alikiba ni mmoja wa wakurugenzi katika lebo hio la Rockstar4000.

Akiongea kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio, Alikiba alifunguka na kusema kwa Barakah The Prince alitoka Rockstar4000 kwasababu ya utovu wa nidhamu.

download latest music    
Barakah The Prince na Alikiba

Kiba alieleza kuwa hakufurahishwa na vitu ambavyo Baraka alikuwa akifanya kwani aliona kuwa mwimbaji huo hakua na heshima kabisa.

“Baraka hayupo Rockstar, alitoka sababu za kukiuka vitu ambavyo hakutakiwa kufanya, Baraka nimemjua baada ya kuwa naye Rockstar400, lakini kiukweli sikufurahishwa na vitu ambavyo alikuwa akifanya, nadhani nilikuwa nikiona kama ni utoto lakini si utoto tena, ni kutokuwa na heshima nikaona haina haja, na mimi nikiwa kama mtu mzima sitakiwi kugombana na mtu mdogo inatakiwa umuache dunia imfunze kidogo, au kama kuna kitu ambacho amefanya au kalishwa sumu basi akapewe dawa itoke,” alisema Alikiba.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere