Alikiba Ataja Familia Kama Chanzo cha Kutomaliza Elimu Yake.

Msanii Alikiba amefunguka na kuweka wazi kuwa katika maisha yake alitamani sana kuwa na elimu kubwa zaidi aliyokuwa nayo lakini hawezi kujutia swala hilo kwa sababu familia yake haikuwa na uwezo kwa kumfanya kumaliza shule kutoka na hali yao kiuchumi,

Akiongea na Big chawa wa Times Fm, Alikiba ansema kuwa hakufanikiwa hata kumaliza kidato cha nne kwa sababu ya hali ya kiuchumi ya nyumbani kwao kipindi alipokuwa akisoma.

download latest music    

sikumaliza form six wala form four  sikumaliza hii ni kwa sababu yamaisha niliyokuwa nikiishi na familia yangu kipindi hicho.-Alisema Kiba.

Hata hivyo kwa sasa alikiba ni moja ya wasanii wakubwa wenye mafanikio na utajiri mkubwa duniani huku akiwa mwenye mafankio na pia mali za kutosha hata kuisaidia familia yake pia.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.