Alikiba Atoa Sababu ya Mofaya Kushindwa Kuingia Sokoni
Msanii Alikiba amefunguka alipokuwa katika mahojiano na Times Fm na kusema kuwa sababu kubwa ya kushindwa kutoka kwa kinywaji chake na kuanza kuonekana sokoni ni dogo sana na siku yoyote kinaweza kuwekwa sokoni.
Alikiba anasema kuwa kila kitu kimekamilika na kwamba imani yake ni kuwa haitachukua muda mrefu kinywaji icho kitaingia sokoni.
OK, tumemaliza kila processs nadhani kuna delay kidogo tu imetokea mabayo inafanya kinywaji kisionekane sokoni lakini nadhani Mwenyezi Mungu akijai hivi karibuni watu wataanza kuiona sokoni na ninaomba waipokee.
Kinywaji icho kilitambulishwa rasmi miezi kadhaaa iliyopita ambapo ilikuwa siku ya ndoa ya msanii huyo hivyo kuwafanya watu kusubiria na kukiulizia kwa muda mrefu kinywaji icho.