Aslay akataa kuwepo kwa Bifu kati yake na Beka

Mwanamuziki wa kizazi kipya Aslay Isihaka akataa kuwepo  kwa bifu kati yake na mwanamuziki mwenzake kutoka Yamoto Band Beka. Wanamuziki hao walisemekana kuingia kwenye ugomvi mara baada ya kundi hilo la Yamoto band kuvunjika na kila mtu kuanza kuimba mwenyewe.

Baada ya kutengana kwa kundi hilo habari za kutoelewana baina ya wanakundi hao zilianza kuenea na ushindani baina yao ulianza  ambapo Aslay alikuwa akiachia nyimbo mpya basi na Beka anaachia nyimbo nyingine hali iliyopelekea tetesi hizo kuzidi kukua katika mitandao ya kijamii.

download latest music    

Katika mahojiano aliyoyafanya Aslay hivi karibu alikataa kuwepo kwa bifu baina yao na kusema yafuatayo:

“Mimi Beka ni mwanangu halafu hatuna tofauti yoyote hadi naondoka huku ananibless mwanangu fanya kitu,ila kuna watu wanatengeneaz genge kwa msanii yoyote anayetoka Yamoto lakini everything is good.watu wanadai mi nataka kumfunika Beka ila sio kweli mi natoa nyimbo kwa maslahi yangu mwenyewe alfu mi siwezi kuwa na na bifu na Beka kwa sababu mi ndo nimempokea Beka na nimemlea na ninamuombea kwa mwenyezi Mungu aendelee kufanikiwa”.

Aslay alikuwa msanii kiongozi na mwenye kipaji ndani ya Yamoto band ambayo iko chini ya Mkubwa Fela ambaye pia ni meneja wa Diamond, baada ya kujitoa kwenye kundi hilo lilisababisha mpasuko hadi watu kudhani kuna ugomvi baina ya wasanii hao. Kwa sasa Aslay ni mwanamuziki wa kujitegemea na anatamba na nyimbo zake zinazofanya vizuri kwenye chati mbalimbali nchini.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.