Aslay na Nandy Wachapwa Faini ya Milioni 5 Kwa Wizi

Msanii wa Bongo fleva Aslay na msanii mwenzake Nandy wanaotamba hivi sasa na wimbo wao wa ‘Subalkheri Mpenzi’ wamejikuta wakichapwa faini ya shilingi milioni tano baada kutuhumiwa Kwa Wizi wa wimbo.

Aslay na Nandy wametawala chati zote za redio na televisheni kwa wimbo wao wa Subalkheri Mpenzi hata juzi juzi hapa walipiga bonge moja la shoo pale escape one lililoitwa Nandy Aslay pamoja na marafiki ambapo watu walijazana kwa ajili ya kwenda kujionea uwezo wa kuimba.

download latest music    

Lakini wiki iliyopita tuliweka habari ya wasanii hawa wawili kuimba wimbo huo bila ruhusa ya wenye wimbo ambao Subalkheri Mpenzi ni wimbo ulioimbwa na kikundi cha taarab asilia visiwani Zanzibar ambao walisema wanataka kuwashataki kwa kuimba wimbo wao bila ruhusa.

Kikundi hiko kilidhamiria kuwaburuza mahakamani wasanii hawa lakini baada ya mazungumzo ya pande zote mbili walifikia uamuzi wa kuwalipisha faini ambayo ni shilingi milioni tano.

Katibu mkuu wa kikundi cha utamaduni wa taarab asilia, Twaha  amefunguka na kusema kuwa licha ya wasanii hao kukiri kosa na kukubali kulipa faini lakini pia meneja wa Aslay ameomba kuingia mkataba na kikundi hicho na kufanya biashara ya kuziimba tena nyimbo zao za zamani ambapo amedai bado hawajakubali kuhusu hilo kwani walishapewa agizo na raisi mstaafu wa awamu ya tatu, Dk. Salmin Amour Juma kuwa wasikubali nyimbo zao za taarab asilia kubadilishwa na kuwa mziki wa kisasa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.