Barakah: Mimi ni Magufuli Wa Bongo Fleva Kutokana na Misimamo yangu Thabiti

Mwanamuziki wa bongo fleva Barakah The Prince amesema yeye ni sawa na Raisi Magufuli kwenye gemu ya  bongo fleva kwa kuwa ana misimamo na itikadi ambazo wengi hawazipendi.

Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa radio, Barakah amesema misimamo yake na kwa jinsi ambavyo hapendi kuona anaonewa, ndio sababu ya watu kutomkubali na ndo sababu ya kuhama hama kwenye uongozi.

download latest music    

Barakah amesema siku zote mtu akiwa na misimamo yake na mitizamo yake binafsi lazima watu watakuona mbaya, huku akimtolea mfano Raisi Magufuli jinsi alivyo na msimamo katika harakati zake za kutetea wanyonge, kitendo ambacho kinapingwa na watu wengi sana katika jamii.

Barakah amekuwa mmoja kati ya wasanii ambaye wamekuwa akikosolewa sana kwenye mitandao ya  kijamii kutokana na maneno yake na misimamo yake hasa akiwa anawaongelea wasanii wenzake.’

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.