Barakah The Prince Achoshwa na Longolongo Kaamua Kufungua Studio Yake

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri hivi sasa na ngoma yake ya ‘sometimes’ amefunguka kuwa amechoshwa na longolongo za label mbalimbali alizofanya nazo kazi mwanzoni huvyo kufikia uamuzi wa kufungua label yake mwenyewe inayoitwa Bana Music.

Mwaka huu umekuwa mgumu kidogo kwa Barakah kikazi kwani aliondoka kwenye moja ya label kubwa Africa Rockstar 4000 kwa like alichodai ilikuwa inamchelewesha kutoa kazi zake. Baada ya kutoa wimbo wake mpya wa ‘sometimes’ Barakah aliingia tena kwenye mgogoro na label yake ya zamani kwa kile alichodai kuwa wanamfanyia hila ili kazi zake zisifanikiwe na pia alimtuhumu maneja wake wa zamani anayejulikana kama Seven kuwa anamharibia akaunti yake ya YouTube ili watu wasiangalie kazi zake.

download latest music    

Barakah ametangaza ujio wa label yake hiyo inayojulikana kama Bana Music Records, aliyoshirikiana na mwanamuziki mwenzake na pia mpenzi wake Naj.

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na Dizzim Online Barakah amefunguka kuwa ni kweli amekuwa akifanya kazi na watayarishaji na studio ambazo zinamhitaji na anazozihitaji kulingana na mahitaji;

Nimeamua sasa niliweke wazi kwa sababu watu wananionq nafanya kazi studio tofauti na wanajiuliza maswali mengi, Studio za Baba music zipo katika umaliziaji na hivi karibuni itaanza kufanya kazi na kutoa kazi zenye ubora. Kutoa kazi zenye ubora ndicho kitu tunazingatia na ninaamini utayarishaji wetu utazingatia kile ambacho mashabiki watahitaji kusikia”.

Lakini pia Barakah ameweka wazi kuwa mbali na kuwa mmoja wa waanzilishi wa studio hizo za Bana music, wapo wasimamizi wenye vigezo ambao wanasimamia label hiyo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.