Barnaba Aachia Albamu Yake Ya Gold Adai Imemgharimu Mil.140

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayetamba kwa vocals kali Barnaba Boy ‘Classic’ ameachia albamu yake rasmi na ameweka wazi kuwa imemgharimu jumla ya milioni 140.

Siku ya jana Barnaba alifanya uzinduzi wa Albamu Yake katika hoteli ya Sea Cliff ambapo hafla hiyo ilihudhuriwa na wasanii mbali mbali wa Bongo fleva na Bongo Movie Lakini pia  na wadau.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Barnaba amefunguka kuhusu maandalizi ya Albamu hiyo yaliyomchukua miaka mitatu na fedha takribani milioni 140:

Hii Albamu imenitesa sana nimeiandaa kwa miaka mitatu na nimetunia pesa nyingi sana nikiongea kwa haraka haraka imenigharimu kama milioni mia na arobaini hivyo naomba mashabiki, vijana wenzangu waweze kunisapoti ili pesa yangu iweze kurudi”.

Kwenye uzinduzi wa Albamu hiyo Msanii wa Bongo movie Jacqueline Wolper alikuwa kivutio baada ya kununua albamu moja kwa dola za kimarekani 3000$ ambayo ni sawa na milioni Sita na laki nane.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.