Barnaba Atoa Tamko Rasmi Kuhusu Mahusiano Yake

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na albamu yake ya ‘Gold’ Barnaba Elias amefunguka na kuwataka mashabiki zake waache kuhoji kuhusu Mahusiano Yake.

Maisha binafsi ya Mahusiano ya Barnaba yalitwala mitandao ya kijamii baada wanawake watatu tofauti tofauti Kulilia Penzi la staa huyo huku kila mmoja akidai ni mpenzi wake.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na gazeti la Dimba, Barnaba alisema amekuwa akikutana na majibizano mengi kumhusu yeye na maisha yake ya mapenzi huku akisema hayo ni mambo yake binafsi hivyo watu wasiyahoji.

Watanzania wananidai muziki mzuri na kazi yangu ni kuwapa kile wanachokipenda..sasa siwezi kuchanganya na maisha yangu mengine..hayo yatabaki kuwa siri”.

Barnaba ameongeza kuwa anachofahamu kwa sasa anatakiwa kuutengeneza muziki wake ufike mbali zaidi kwa kuwa bado ana deni kubwa kwa mashabiki zake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.