Barnaba Boy Azidi Kulia na Kuumizwa na Penzi la Mzazi Mwenziye

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayetamba kwa uwezo wake wa kupanga mashairi na kuandika, Barnabas boy classic amefunguka maneno mazito kwa mzazi mwenzie anayejulikana kama Zuu.

Barnaba na Zuu walikuwa na uhusiano kwa muda mrefu na hata kubarikiwa kuzaa mtoto mmoja wa kiume anayeitwa Steven. Lakini wawili hao waliachana. Pamoja na kuachana na Zuu, Barnaba amezidi kuteswa na penzi lake licha ya kuachwa kwenye mataa na Zuu kumpa penzi mwanamuziki wa bongo fleva ambaye ni underground anayejulikana kama Brown. Ambapo inasemekana Barnaba aliingia studio na kutoa kibao cha ‘Mapenzi jeneza’ ambapo mashairi yake yanasema ‘Nilimpenda miaka tisa penzi la miezi sita likakatiza Upendo, chuki akazidisha na kuyahamisha malengo’.

download latest music    

Siku ya Jana ilikuwa ni kumbukumbu ya kuzaliwa Zuu na Barnaba kupitia ukurasa wake wa Instagram alifunguka yafuatayo;

Wewe ni rafiki yangu na ndugu yangu na uvungu wa moyo wangu nakushukuru kwa kuwa daraja kwenye maisha yangu nashukuru nimevuka Salama, matatizo ni sehemu ya kila mwanadamu, upendo wangu juu ya zawadi uliyonipatia iko pale pale (Steve) na kitu kizuri ninakuheshimu sana mbali na mambo yote na kitu kingine furaha yangu kukuona kutabasamu hata kama hilo tabasamu silitengenezi mimi lakini angali unatabasamu basi nafurahi kukuona, nakutakia maisha mema yenye baraka nawaombea heri katika familia yako nakuombea heri na uwahi uwe shuhuda wangu nami niwe shuhuda wako Wa kila jambo heri. Heri ya kuzaliwa Mama Steve, mama watoto , mzazi mwenzangu damu ya Yesu ikuangaze milele”.

Barnaba na Zuu waliachana baada ya kuwa wrote kwa miaka mingi, baada ya kuweka ujumbe huu mashabiki wengi walijitokeza na kumshauri Barnaba arudiane na Zuu ili walee mtoto wao.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.