Ben Pol Akana Kuwa Kwenye Penzi na Ebitoke

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Bernard Paul maarufu kama Ben Pol amekana kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na mchekeshaji kutoka Timamu Tv, Ebitoke.

Tetesi za Ben Pol na Ebitoke kuwa Kwenye Mahusiano zilianza kusikika Mara baada ya Ebitoke kukiri hadharani kuwa anampenda Ben Pol na kuwa angefurahi sana kuwa naye.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Ben Pol alikataa kukubali kuwa Kwenye Mahusiano na Ebitoke au hata kuwahi kuwa naye tofauti na Ebitoke ambaye ameshasema mara kwa mara kuwa wapo Kwenye Mahusiano:

Kuhusiana na mahusiano hayo its Complicated ingawa kila kitu nilishaongea ila kila kitu kilichoonekana kwenye vyombo vya habari ni sehemu ya maisha yangu”.

Lakini pia Ben Pol alifunguka na kuendelea kunena:

Vyovyote mtu atakavyohisi aendelee kuhisi ila mimi siwezi kutamka chochote ila muda ukifika kama kweli niko kwenye mahusiano ntaweka wazi na kama siko nae pia itafahamika”.

Imeshawahi kusemekana kuwa Ben Pol hajawahi hata kuwa Kwenye Mahusiano na Ebitoke bali ilikuwa ni kiki tu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.