Brown Akanusha Kukimbia Mombasa Baada Ya Kuiba Mke Wa Mtu

Msanii wa muziki kutoka Mombasa Kenya, Brown Mauzo ameibuka na kukataa yuhuma zinazomkabili za kukimbia Mombasa na kuja Dar Es Salaam baada Ya kuiba mke wa mtu.

Tuhuma hizo za Brown kukimbia Mombasa zilitolewa na msanii mwenzake anayeitwa Kelechi ambaye alidai Msanii huyo alikimbilia Dar kutoka Mombasa baada ya kutembea na mke wa Meneja wake.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Kipindi cha Enews cha East Africa Tv, Brown amekataa tuhuma hizo na kusema yeye na Meneja wake wapo vizuri kabisa na hajaiba mke wake wala hajakimbia Mombasa.

Yaani hakuna kitu kama hicho kama sio naweza kupiga simu hata saa hii kwa meneja wangu niongee naye, hayo ni maneno watu tu wanazungumza yaani hilo jambo ndio kwanza nalisikia sasa hivi”.

Lakini pia Brown amesisitiza kuwa yeye yupo hapa Dar kwa muda na nyumbani Kenya anaweza kurudi lakini sio kwamba amefukuzwa kwa sababu ya kuiba mke wa Meneja wake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.