Casto Dickson Afuta Rasmi Tatoo Ya Tunda

Mtangazaji wa Kipindi cha Siz Kitaa cha Clouds Tv Casto Dickson ‘Mwananchi Wa Kawaida’ hatimaye amefuta tattoo ya aliyekuwa Mpenzi Wake video vixen Tunda Sebastian.

Mwaka jana wakati Tunda na Casto walipokuwa kwenye mapenzi mazito, Casto alifikia uamuzi kwa kwenda kuchora tattoo kubwa mkononi ya jina la Tunda.

download latest music    

Lakini tattoo hiyo ilikuja kuwa changamoto kwake kwani Baada ya miezi michache Penzi hilo lilifika kikomo na Tunda alionekana akiwa na mwanaume na kumuacha Casto na tattoo hiyo.

Ingawa Mwanzoni Casto alisema hataweza kuifuta tattoo hiyo lakini Hivi sasa ameonekana kubadilisha maamuzi yake kwani amefuta tattoo hiyo kwa kuchora picha juu ya jina Tunda.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.