Chegge- Nimeumizwa na Kifo Cha Agnes Masogange

Mwanamuziki wa Bongo fleva Said Juma ‘Chege Chigunda’ ameongelea kifo cha msanii wa filamu na video queen Agnes Gerald ‘Masogange’ na kusema hatokaa amsahau mrembo huyo.

Masogange alifariki dunia Ijumaa iliyopita katika kituo cha Huduma za Afya cha Mama Ngoma kilichopo Mwenge jijini Dar ambapo jana aliagwa katika Viwanja vya Leaders na kusafirishwa kwenda kwao Mbeya ambako alizikwa jana Aprili 24, 2018 kijijini kwao Utengule, Mbalizi.

download latest music    

Chege aliyasema hayo juzi Jumapili alipokuwa Viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar katika kuuaga mwili wa Masogange aliyefariki ghafla baada ya kupungukiwa damu.

Kiukweli msiba umeniumiza kama msanii kwani sisi ni miongoni mwa wasanii wa Bongo Fleva wa mwanzomwanzo kumtoa Masogange kimuziki, kifupi sitamsahau na nawapa pole ndugu na wanafamilia”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.