Chemical- Nina Bahati Ya Kutongozwa Sana na Wanaume

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayetamba kwa michano yake ya rap, Chemical amefunguka na kuweka wazi kuwa anatongozwa sana na wanaume tofauti na watu wanavyodhania.

Katika Interview yake  aliyofanya na kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv, Chemical amesema ana Bahati ya kukutana na wanaume kibao na anatongozwa kuliko watu wanavyomfikiria kwamba ana swagga za kiume.

download latest music    

Mimi Nina Bahati ya kukutana na wanaume wengi ambao wananitongoza kwa sababu unakutana na mwanaume mwingine anasema kabisa kuwa anapenda mwanamke ambaye anaonekana kama mpambanaji ambaye mnaweza kufight wote katika maisha watu wa namna hiyo wapo wengi.

Kuna watu wanaamini Chemical hatongozwi, Mimi natongozwa sana huko kwenye DM kwa sababu pamoja na vyote hivi mimi bado ni mwanamke na nina Boyfriend ambaye anavutiwa na hivi nilivyo kaa kiume kwa sababu sio kila mwanaume anapenda mwanamke anayeweka makucha marefu na kuvaa mawigi”.

Chemical amewataka watu waondoe dhana ya kwamba mwanamke akivaa kiume basi ndio anataka kuwa mwanaume Hapana hayo yanakuwa ni mavazi tu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.