Chid Benz Akana Kuiga Staili Ya Nywele

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Radhi Makwiro maarufu kama Chid Benz amefunguka na Kukana kabisa tuhuma za kuiga staii yake mpya ya nywele.

Wikiend iliyopita Chid Benz aliibukia pande za Tandale ambapo alipiga shoo Kwenye charity event ya Msanii Diamond Platnumz ndipo alipoonekana kapaka rangi nywele zake.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers,  Chid Benz ametajwa sababu ya kupaka  nywele zake rangi na sio kwamba anawaiga wasanii wanaotoka katika jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC) bali wakati wake umefika wa kubadilika kichwani.

Unajua watu wanafikra tofauti na kupenda kuongea mambo mengi, mtu anapofanya kitu wanahisi tu atakuwa amewaiga watu wengine lakini mimi nimeamua kufanya hivi kwa kuwa wakati kwa upande wangu umefika”.

Lakini pia Chid Benz alimpongeza Diamond kwa kusema amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuufikisha Muziki wa Bongo Fleva mbali.

Namuombea Diamond aendelee kupenda kazi yake kwani Muziki wa Bongo Fleva unafanya mengi mazuri tuu, kwa hatua alioifanya namuombea kwa Mungu azidi kufika mbali, mbali zaidi“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.