Chiddi Mapenzi Ajibu Tetesi Za Kumwagana na Shamsa Ford

Mfanyabiashara maarufu kwenye mitandao ya kijamii Chiddi Mapenzi amefungukia tetesi za kuachana na mke wake  ambaye ni muigizaji wa  Bongo movie Shamsa Ford.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha FNL cha East Africa Tv, Chiddi amesema kuwa msanii huyo bado ni mke wake na hajaamua kumpost kwasababu yuko busy kwasababu anatarajia kufungua duka lake mwezi ujao.

download latest music    

Shamsa ni mke wangu sio kwamba hapost, labda mwenyewe kaamua ana mambo yake lakini by the way anafungua duka lake soon mwezi ujao la kike kwahiyo hakuna tatizo lolote la kike nipo nae mama”.

Lakini pia Chiddi aliendeleq kutetea mahusiano yake na Shamsa:

Unajua watu wengine wamezoea kupostiana sasa mimi siko hivyo wewe unanijua ndugu yangu, mimi mtu mzima siko hivyo mimi niko nae sema nilikuwa sipo nilikuwa safari juzi kati tu, kwahiyo mama niko nae sema yuko busy anataka kufungua ofisi yake anashinda dukani kwake”.

Tetesi Za Shamsa kuachana na Chiddi zilianza Baada ya Msanii huyo kujiposti akiwa na majeraha usoni yaliyopelekea Tetesi Za kupigwa na Mume Wake Lakini pia amekuwa akiweka vijembe vinavyozaniwa kumuelekea Mume Wake huyo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.