Chuchu Awapa Makavu Wote Waliomsema Ray Kama Tasa na Muathirika

Muigizaji wa Bongo movie Chuchu Hansy ambaye pia ni mzazi mwenza wa staa wa Bongo movie Ray Kigosi amewatolea uvivu watu wote waliokuwa wanamsema Ray kuwa ni tasa hana uwezo wa kuzaa na pia muathirika wa Ukimwi.

Ray na Chuchu wamezaa kwa pamoja mtoto wao wa kiume anayeitwa Jaden, lakini amedai kabla hawajazaa mtoto wao Ray alikuwa mtu ambaye alisemwa sana na watu.

download latest music    
Ray na mtoto wake Jaden

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Chuchu amefunguka haya:

Jaden Vincent Kigosi Asante Mungu najua umejua kumkomesha vibaya baba yako najua waja walikuwa wanaongea mengi juu ya ujio wako na kabla ya ujio wako walikuwa wanasema mengi hata mimba yako nilisemwa mengi leo nimetoa kidogo ya moyoni, Miungu watu walianza kusema juu ya Baba yako mara oooh Ray hazai angekuwa anazaa sahivi angekuwa na mtoto baadae wakahamia kwangu baada ya kuharibika sura nilivyokuwa na ujauzito mara mgonjwa wa Ukimwi na mengine mengi.

Nilivyozaa wakaendelea kumsingizia Ray hawezi kuzaa mtoto na sio wake sijui Kazaa na mzungu mara mwarabu rafiki wa Ray ilimradi kutapatapa yote haya nikayavumilia na yakapita”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.