Davina- Baada Ya Kuachika Sana Kwenye Ndoa Nimejifunza Mengi

Muigizaji mkongwe wa Bongo movie Halima Yahaya amefunguka na kudai kuwa pamoja na kwamba ameachiwa sana kwenye ndoa zote alizowahi Kuolewa lakini amejifunza mambo mengi kupitia huko.

Davina amekiri kuwa ni kweli hajawahi kupata bahati ya kukaa na mume kwa muda mrefu lakini amejifunza kuwa mwanamke jasiri na shupa I na kuweza kujua kuwa kujituma na kuweza kuwalea watoto wake mwenyewe.

download latest music    

Kwenye mahojiano  na Amani kwa njia ya simu, Davian alisema Mungu amemjalia kupitia kwenye ndoa mbili lakini hakubahatika kukaa kwa muda mrefu lakini kikubwa ni kwamba ndoa hizo zimemfunza mambo mengi sana ya kujituma ili aweze kuwalea watoto wake vizuri.

Siwezi kujilaumu hata siku moja kwa nini sikai kwenye ndoa zote nilizozipitia bali ninachojua ni kwamba zimenifundisha mambo mengi sana hasa ya kujisimamia mimi kama mimi na kuendesha familia nikiwa kama mwanamke mwenyewe bila mtu mwingine pembeni”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.