“Daxo Chali Alikuwa Aliniimbisha Muziki Siujui”- Nini

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na ngoma yake ya Kolo, Mwanadada Nini ameibuka na kudai Daxo Chali alikuwa hajamjulia mziki wake wa kufanya kwani alikuwa anaimba nyimbo za ajabu.

Kama utakumbuka Nini alikuwa yupo chini ya label ya MJ Records chini ya Producer Daxo Chali lakini aliishia kutimuliwa baada ya kudaiwa kuwa na utovu wa nidhamu.

download latest music    

Baada ya kuondoka Kwa MJ Records, hivi sasa Nini yupo chini ya uongozi wa Nay wa Mitego ambapo amedai ndipo alipopatia umaarufu zaidi na muziki wake kujulikana zaidi kwani anafanya muziki mzuri.

Kwenye mahojiano na Enews ya East Africa Tv, Nini amedai kuwa mziki aliokuwa anaimba chini ya uangalizi wa Daxo CHali haukuwa muziki sahihi kwake na wala alikuwa haujui wala haupendi.

Mashabiki zangu wameongezeka kwa sababu mziki ninaoinba sasa ni tofauti na niliokuwa naomba kwa Daxo Chali kwa sababu mziki ninaoinba sahivi ni ule mziki ambao Watanzania wameshazoea kuusikia na kuupenda na  mimi nafurahia zaidi kuimba stabilizer hii ya hivi sasa”.

Kumekuwa na tetesi kuwa Nini anatoka kimapenzi na Nay wa Mitego, taarifa ambazo mwenyewe amezikataa kabisa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.