Diamond Akiri Kuwa Bado Hajajua Atakuwa na Nani ‘Valentines Day’

Mwanamuziki wa Bongo fleva na mmiliki wa label ya WCB, Diamond Platnumz amefunguka na kukiri kuwa bado hajajua mipango yake ya Valentine’s Day imekaaje mpaka hivi sasa.

Ikiwa siku ya Wapendanao ‘Valentines Day’ ili njiani inakuja siku ya kesho tarehe Kumi na nne ambayo ni siku maalumu kwa wale wapendanao ikiwa ni sherehe inayosheherekewa dunia nzima.

download latest music    

Diamond ambaye ametengeneza headlines kila kona kwa wiki hizi chache zilizopita ambapo kila mwanamke anasemekana katoka naye kuanzia Mia aliyesambaza video clip akiwa Madale, mpaka kwa Wema aliyeonekana akipeana mabusu hadharani mpaka kwa Tunda ambaye amesemekana ana ujauzito wake lakini yupo Zari.

Zari ndio mwanamke pekee ambaye Diamond amemkubali kuwa anaweza kusheherekea naye sikukuu ya wapendanao siku ya kesho.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Dizzim Online Diamond alifunguka na kusema kuwa hajajua atasherekea nani mpaka hivi sasa labda atajua ikifika siku yenyewe:

Sasa itategemea Valentines yenyewe itanikutia wapi kama itanikutia South Africa kwa mzazi mwenzangu basi atakuwa yeye lakini pia kama itanikutia hapa Tanzania basi Valentines wangu watakuwa ndugu zangu na marafiki zangu”.

Lakini pia Diamond ameendelea kuwasihi Watanzania wampokee Mbosso vizuri na wampe sapoti yao yote.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.