Diamond Adaiwa Kuonekana Akiwa na Video Queen Irene

Mwanamuziki Diamond Platnumz ameingia tena kwenye vichwa vya habari leo baada ya stori za chini ya kapeti kudai kuwa ameonekana na model na video vixen mrembo Irene. Ikiwa ni wiki kadhaa tangu Diamond akiri kuzaa na Hamisa Mobetto na hatimaye kusamehewa na mzazi mwenzie Zari Diamond yupo tena kwenye maji ya moto.

Habari zinazoenea kwa kasi ya ajabu zinadai kuwa Diamond aliyekuwa nchini Afrika ya Kusini tangu wiki iliyopita kwaajili ya sherehe ya kuzaliwa ya mpenzi wake Zari, alionekana tena sehemu nyingine na Mrembo Irene ambaye na yeye alikuwa nchini humo kwa ajili ya kazi na kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.

download latest music    

Pamoja na kuwa Diamond alikataa kuwa na uhusiano na mrembo toka Namibia Dillish, lakini stori za udaku zinadai kuwa walikuwa wote na pia dada huyo ni mjamzito ingawa yeye mwenyewe hajathibitisha kuwa mjamzito.

Diamond na Irene wamewahi kuongelewa kama wako pamoja kipindi cha nyuma yaani kulikuwa na tetesi kuwa diamond alikuwa anachepuka na binti huyo mrembo na hata ilisemekana kuwa binti huyo alishika ujauzito wa Diamond ingawa alipohojiwa alikataa na kusema yeye anampenda Zari na yuko na Zari hivyo habari hizo ni za uongo na zinaenezwa na wabaya wake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.